Skip to main content

Malengo Ya Maendeleo Endelevu Na Wajibu Wa Serikali Za Mitaa

Imechapishwa na Policy Forum

Ndugu Msomaji, tunafurahi kwa mara nyingine kukuletea kitabu kipya kiitwacho “Malengo ya Maendeleo Endelevu na Wajibu wa Serikali za Mitaa” ikiwa ni mwendelezo wa mkakati wa Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Jukwaa la Sera (PF-LGWG) kwa kuelimisha wananchi kuhusu sera za kitaifa na kimataifa zinazopaswa kutekelezwa na Serikali za Mitaa ili kuhamasisha ushiriki wa
wananchi kwenye masuala ya umma na kukuza uwajibikaji katika jamii.

Maazimio Na Mapendekezo Ya Waheshimiwa Madiwani Baada Ya Kushiriki Mafunzo Ya Uongozi Na Uwajibikaji Wa Kijamii

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi Waheshimiwa madiwani tulioshiriki warsha ya mafunzo ya uongozi na uwajibikaji wa kijamii iliyoandaliwa na kuratibiwa na Kinkundi kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum kwa kushirikiana na halmashauri ya Kiteto kati ya tarehe 18 hadi 23 Julai 2016,

Baada ya kupokea na kujadili mada mbalimbali, tumetambua umuhimu wa nyaraka na taarifa mbalimbali kwenye hatua zote za usimamizi wa rasilimali za umma na mfumo wa uwajibikaji jamii,

Taarifa ya Ufuatiliaji wa Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Oktoba 25, 2015

Imechapishwa na Policy Forum

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kwa kushirikiana na Policy Forum, ilifuatilia mchakato wa uchaguzi mkuu wa Tanzania wa mwaka 2015 katika mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na Mwanza. Lengo kuu la ufuatiliaji huo lilikuwa ni kutathimini uzingatiaji wa misingi ya kidemokraisa, haki za binadamu, na utawala bora kwenye mchakato mzima wa uchaguzi mkuu wa 2015. Kusoma zaidi bofya hapa.

Tangazo la Kifo: Mungu Akulaze Mahali Pema Peponi Alex Modest Ruchyahinduru

Imechapishwa na Policy Forum

Sekretariati ya Policy Forum inasikitika  kutangaza kifo cha Alex Modest Ruchyahinduru, meneja wetu wa Mawasiliano na Uchechemuzi, aliyefariki asubuhi ya leo Mei Mosi 2016 katika hospitali ya Aga Khan mjini Dar es Salaam. Baadhi yenu huenda mlikuwa na taarifa za kulazwa kwake kufuatia operesheni ya kichwa iliyofanyika kipindi cha Pasaka takriban mwezi mmoja uliyopita. Alex alijiunga na Policy Forum Machi 2009.

Mtazamo wa Azaki Kuhusu Siku 100 za Magufuli Madarakani

Imechapishwa na Policy Forum

Kabla ya uchaguzi mkuu  wa Oktoba 25, 2015, Asasi Za Kiraia (AZAKI) chini ya Kikundi Kazi  cha Bajeti cha  Policy Forum ziliandaa na kuwasilisha kijarida kinachoitwa“Vipaumbele  Vyetu Vikuu  kwa Serikali Ijayo”  kwa  vyama mbalimbali vya siasa  vilivyokuwa vinashiriki katika uchaguzi ili kutilia mkazo yaliyomo kwenye kijitabu hicho.  Kijarida hicho kilikuwa na masuala nyeti yaliyohitaji serikali ya awamu ya tano kuzingatia.  

Mjue Diwani (Toleo la Pili)

Imechapishwa na Policy Forum

Ndugu msomaji, tunayo furaha kukuletea kitabu kipya kiitwacho “Mjue Diwani”  ikiwa ni mwendelezo wa mkakati wetu wa kikundi kazi cha serikali za mitaa wa kuwaelimisha wananchi kuhusu utawala wa Serikali za Mitaa na kukuza uwajibikaji katika jamii. Kusoma zaidi bofya hapa

Tamko La Asasi Za Kiraia Kuhusu Viashiria Vya Uvunjifu Wa Amani Wiki Moja Kuelekea Tarehe Ya Upigaji Kura Katika Uchaguzi Mkuu Tanzania Tarehe 25.10.2015

Imechapishwa na Policy Forum

Asasi za Tanzania tumeendelea kufuatilia mchakato wa uchaguzi mkuu 2015 tangu uandikishaji wapiga kura, uhamasishaji hadi kampeni zinazoendelea kwa umakini mkubwa. AZAKI tumefanya hivyo tukiamini kuwa uchaguzi  ni sehemu kuu ya michakato ya kidemokrasia hapa nchini kama ilivyo duniani kote. Sisi asasi za kiraia Tanzania, tukiwa watetezi na wasimamizi wa demokrasia, utawala bora na haki za binadamu, hatumuungi mkono mgombea yeyote wala chama chochote cha kisiasa kinachotafuta kuingia madarakani wala hatulengi kuchukua dola.

Maswali Yetu Muhimu kwa Serikali ya Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Mfumo wa Uongozi / utawala wa sasa wa Tanzania utafikia mwisho wake katika miezi michache ijayo. Hii inatoa njia kwa mfumo mpya kuchukua hatamu ikitegemewa kuwa na mikakati mipya au iliyoboreshwa kusukuma maendeleo ya kiuchumi.

Makosa ya Rushwa Katika Chaguzi Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tunakuletea tena chapisho hili la tatu katika mtiririko wa machapisho yanayohusu elimu kwa umma juu ya kupambana na rushwa.
Mtakumbuka kuwa chapisho letu la kwanza la pamoja lilihusu sheria mpya namba 11 ya mwaka 2007 ya kuzuia na kupambana na rushwa hapa Tanzania,

Chapisho hili linaweka wazi sheria zetu zinavyosema kuhusu makosa yarushwa katika chaguzi hapa nchini Tanzania na adhabu zinazotolewa kwa makosa husika,

Subscribe to Resources