Skip to main content

Tanzania Forest Conservation Group (TFCG)

Imechapishwa na Policy Forum

Tanzania Forest Conservation Group  (TFCG) ilianzishwa mnamo 1985. Kwa zaidi ya uzoefu wa miaka 20, sisi ndio shirika kubwa zaidi lisilo la kiserikali la Tanzania linalozingatia uhifadhi wa misitu ya asili.

Kwa miaka mingi, timu yetu imegundua kuwa njia bora zaidi ya kufikia dhamira yetu ni kupitia kujengea wadau uwezo, uchechemuzi na utafiti.

SNV

Imechapishwa na Policy Forum

SNV imekuwepo nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 40. Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2000 uchumi wa Tanzania umekuw akikua katika hali ya kuridhisha. Licha ya ukuaji huu wa uchumi, bado Tanzania inakabiliwa na tatizo la umaskini. kiwango cha umaskini bado kinasimama karibu 34% licha ya ukuaji wa uchumi wa kila mwaka wa karibu 7%.

Promotion of Education Link Organisation (PELO)

Imechapishwa na Policy Forum

Kuanzishwa kwa PELO kulianzia wakati waalimu wawili walikuwa na maswali ya kawaida juu ya kwanini wanafunzi wa Kitanzania wanamaliza masomo ya sekondari wakati hawana uwezo wa kuwasiliana kupitia lugha ya Kiingereza ikilinganishwa na wanafunzi wenzao katika nchi jirani? Walipata wazo la kujumuika kuanzisha shirika ambalo linaweza kuleta majibu ya swali hili na mwishowe PELO ilianzishwa mnamo 1998 na ilisajiliwa mnamo 2000 chini ya sheria ya jamii na nambari ya usajili.

Open Mind Tanzania (OMT)

Imechapishwa na Policy Forum

Open Mind Tanzania (OMT) ni shirika lisilo la kiserikali linaloongozwa na vijana. Inashughulika na kufungua mawazo ya watu, vijana haswa kupitia uchechemuzi shirikishi na ujengaji uwezo katika maeneo ya uwezeshaji wa kisheria, kijamii, na kiuchumi, kuwawezesha (vijana) kuwa wasimamizi wa maendeleo yao na wachangiaji wakuu kwa ustawi wa jamii yao , nchi na ulimwengu kwa jumla. 

Subscribe to Dar es Salaam