Mradi wa “Raia Makini” Kuimarisha Uwajibikaji wa Fedha za Umma Nchini Tanzania
Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability kwa kushirikiana na Policy Forum, imezindua rasmi mradi mpya unaolenga kuimarisha ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa fedha za umma, kupitia juhudi za kuongeza uwazi, uwajibikaji na kupambana na rushwa nchini Tanzania.