Skip to main content

Utawala wa Kidemokrasia katika Jamii

Imechapishwa na Policy Forum

Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa Kiongozi aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa kulingana na mipango na makubaliano ya vikao vya kisheria vya kijiji na mtaa. Kwa taarifa kamili tafadhali bofya hapa.

Kuimarisha Utendaji wa Bunge katika Usimamizi wa Bajeti: Hoja ya Ofisi ya Bajeti ya Bunge

Imechapishwa na Policy Forum

Usimamizi wa Bunge uliohuru unahitaji pawepo na uhalisia wa kutenganisha na kuwa na uwiano mzuri wa mamlaka kati ya Bunge na Serikali.Pale ambapo hakuna mipaka na serikali ikiwa na nguvu kubwa kuliko bunge katika utoaji habari na rasilimali, achilia mbali kamati za usimamizi, haiwezekani kwa bunge kuwa na uwezo wa kuwa na makali endelevu dhidi ya serikali . Kwa kuangalia utendaji wa Usimamizi wa Bajeti ya Bunge katika mazingira haya, hoja ya umuhimu wa kuanzisha Ofisi ya Bajeti ya Bunge inaweza kuibuliwa.

Mkakati wa Pamoja wa Uratibu na Matumizi bora ya Misaada

Imechapishwa na Policy Forum

Mchakato wa kuhalalisha mahusiano baina ya Serikali, wahisani, wafadhili na Asasi zizo za kiserikali AZAKI umekuwa na changamoto nyingi. Kumekew na juhudi nyingi ambazo zimekuwa zikitoa tumaini kwa AZAKI kwamba mahusiano rasmi na wadau wengine wa maendeleo ni jambo ambalo linawezekana kuwa rasmi na endelevu.

Makosa ya Rushwa katika Chaguzi Tanzania

Imechapishwa na Policy Forum

Policy Forum na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) tunakuletea tena chapisho hili la pili katika mtiririko wa machapisho yanayohusu elimu kwa umma juu ya kupambana na rushwa.

Ukuaji wa Uchumi Tanzania: Je, Unapunguza Umaskini?

Imechapishwa na Policy Forum

Tanzania imesifiwa sana kuwa inaendesha uchumi wake katika njia sahihi. Katika chapisho la hivi karibuni, “Tanzania: the story of an African transition”, shirika la fedha duniani IMF, linadai kuwa katika miongo miwili iliyopita, uchumi wa Tanzania umepitia kipindi cha mpito chenye mafanikio, ambapo uchumi huria na mageuzi ya kitaasisi yamepelekea kuongezeka kwa pato la taifa hadi kufikia zaidi ya 7% kwa mwaka tangu 2000. bofya hapa

Taarifa Ya Hali Ya Uchumi Wa Taifa Kwa Mwaka 2008 Na Malengo Katika Kipindi Cha Muda Wa Kati (2009/10-2011/12)

Imechapishwa na Policy Forum

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa likae kama Kamati ili liweze kupokea na kujadili Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa katika kipindi cha mwaka 2008 na malengo katika kipindi cha Muda wa Kati (2009/10 – 2011/12). Pamoja na hotuba hii, nawasilisha Kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2008; na Kitabu cha Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2009/10. bofya hapa

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania - Mwongozo wa Jamii za Kiraia

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti kwa kawaida imekuwa ikichukuliwa kuwa ni kazi ya wataalamu, wachumi na wahasibu tu. Lakini uamuzi wa Serikali wa namna gani ya kukusanya mapato huwaathiri wananchi wote. Kiwango cha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kodi nyingine huathiri bei za vitu vinavyotumiwa katika kaya. Uamuzi wa matumizi ya serikali ndio huweka wazi iwapo viwango vya mishahara ya walimuna iwapo kutakuwa na dawa na vifaa vya kutosha katika zahanati au la.

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania - Mwongozo wa Jamii za Kiraia

Imechapishwa na Policy Forum

Bajeti kwa kawaida imekuwa ikichukuliwa kuwa ni kazi ya wataalamu, wachumi na wahasibu tu. Lakini uamuzi wa Serikali wa namna gani ya kukusanya mapato huwaathiri wananchi wote. Kiwango cha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kodi nyingine huathiri bei za vitu vinavyotumiwa katika kaya. Uamuzi wa matumizi ya serikali ndio huweka wazi iwapo viwango vya mishahara ya walimuna iwapo kutakuwa na dawa na vifaa vya kutosha katika zahanati au la.

Tamko La Asasi Za Kiraia Juu Ya Mafanikio Na Madhara Kwa Tanzania Kuendelea Kutumia Ushauri Wa IMF

Imechapishwa na Policy Forum

Sisi wajumbe wa Asasi za kiraia za ki-Tanzania tuliokutana leo ukumbi wa Dar es Salaam International Conference Centre, tarehe 10 Machi 2009 kwa uratibu wa mtandao wa Policy Forum, Human Development Trust na Tanzania AIDs Forum, baada ya kujadili na kutafakari kwa kina taarifa za ''mafanikio'' ya utekelezaji mipango ya IMF na sera za Tanzania ki-uchumi kwa miaka ya 2000 hadi 2008 tumebaini yafuatayo:-

1. Ni kweli takwimu zinaonesha kukua kwa uchumi kwa wastani wa zaidi ya asilimia 7% kwa kipindi tajwa,

Nioneshe Pesa Ziliko

Imechapishwa na Policy Forum

Katika miezi ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la madai ya uwajibikaji kutoka kwa Wabunge ambayo yamebadilisha muonekano wa Bunge na yamepelekea kujiuzuru kwa mawaziri kadhaa, ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu. Mswada wa Sheria ya Ukaguzi imepelekwa Bungeni chini ya hati ya dharura na itajadiliwa katika kikao kijacho cha Bajeti mwaka huu. Mswada huu unalenga kuiongezea Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAO) uhuru mkubwa wa kutoingiliwa na Dola katika utendaji wake wa kumsaidia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Subscribe to Resources