Nchi yetu imekuwa ikifanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali wakiwemo Rais, Wabunge na Madiwani kila baada ya miaka mitano au kwa mujibu wa sheria pale itakapo hitajika. Wananchi hupata nafasi ya kuelimishwa umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa kupiga kura au kuwa wagombea wa nafasi mbalimbali. Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni haki ya msingi inayotolewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tamisemi Kushirikiana na AZAKI kuandaa Mwongozo wa Utoaji na Usimamizi wa Mikopo kwa Vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu Wenye Ulemavu
Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017-2020/21), pamoja na malengo mengine, unakusudia kuweka mazingira wezeshi kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujiajiri na kushiriki katika shughuli za kimaendeleo kama vile uvuvi, kilimo, ufugaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
Miongoni mwa mikakati iliyowekwa na Serikali ya kutimiza lengo la kusaidia makundi hayo ni utoaji wa mikopo isiyo na riba.