Mkurugenzi wa TAKUKURU Afurahishwa na Kampeni ya Kudhibiti Upotevu wa Fedha za Umma
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema imefurahishwa na kampeni ya Policy Forum iitwayo Stop the Bleeding ambayo inahusu udhibiti wa upotevu wa fedha za Umma kupitia njia haramu zikiwemo utakatishaji wa fedha na ukwepaji kodi. Hayo yamesemwa Novemba 11, 2018 Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Diwani Athumani alipokuwa akiongea na Wabunge wa Bunge Tanzania Wanaopamba na Rushwa (APNAC).