Skip to main content
Imechapishwa na Policy Forum

Februari 2015 Jopo la Ngazi ya Juu Kuhusu Uhamishaji Haramu wa Fedha kutoka Barani Afrika, likiongozwa na Mwenyekiti wake Rais Thabo Mbeki, liliwasilisha ripoti yake kwa Tume ya Umoja wa Afrika/Tume ya Umoja wa Kimataifa ya Kiuchumi Barani Afrika (AUC/ECA). Ripoti ilionesha kuwa nchi za Kiafrika hupoteza kwa wastani dola bilioni 50 kwa mwaka kutokana na uhamishaji haramu wa fedha. Shughuli za kibiashara za sekta binafsi ndizo zinazochangia kwa kiwango kikubwa uhamishaji haramu wa fedha (IFFs), zikifuatiliwa na uhalifu uliopangwa, kisha shughuli za sekta ya umma. Vitendo vya rushwa vinachukua nafasi kubwa katika kuwezesha
uhamishaji huu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Makampuni ya Kimataifa huhamisha faida kwa makampuni tanzu yenye kodi ndogo au mamlaka za kisiri ambapo mara nyingi hayo makampuni tanzu ni makampuni hewa, mengi yakiwa na mwajiriwa mmoja au wawili tu, wakati shughuli zilizo nyingi hufanyika katika nchi nyingine. kusoma zaidi bofya hapa.