Skip to main content
Submitted by Web Master on 24 August 2017

Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ina alama 53 kati ya alama 100 za RGI 2017. Tofauti na sekta ya madini ambayo ni kongwe, Tanzania bado haijaanza uzalishaji mkubwa wa gesi baada ya ugunduzi wa gesi nyingi katika kina kirefucha bahari ya Hindi  ambayo hivi sasa inakadiriwa kuwa futi za ujazo trilioni 57. Hali ya kuridhisha ya Tanzania katika uwezekano wa kupata thamani ya rasilimali, kipengele kinachopima ubora wa utawala katika utoaji wa leseni, mfumo wa kodi, athari kwa jamii na ushiriki wa Serikali, hutegemea sana utaratibu wa kisheria wenye masharti mahimu kuhusu utawala na uwazi. Kwa kuwa Tanzania bado haijaanza uzalishaji mkubwa wa gesi na kuuza nje ya nchi, sheria husika nyingi zikiwa ni mpya hazijatekelezwa kikamilifu kuwezesha tathmini ya ufanisi wake. Kutegemea hali ya uwekezaji na utekelezaji wa sera, sheria na kanuni husika, tasnia ya mafuta na gesi vina uwezo wa kuleta
manufaa makubwa kwa Tanzania moja kati ya nchi zenye ongezeko kubwa la watu duniani. Soma Zaidi ...